
Katika nyakati hizi tulizopo sio kitu kigeni masikioni kusikia mtoto kabakwa au kanajisiwa, kauawa na dada wa kazi au kaibwa. Yaani kesi ni chungu nzima. Mambo ni magumu kiasi kwamba wazazi wanaishi kwa hofu juu ya watoto wao. Kama wewe ni mzazi na unamwamini Mungu Aliye hai katika Kristo Yesu basi huna haja ya kuogopa kwa sababu ya Jina hili la fahari na lenye kutisha. Watoto hao aliokupa Bwana wanalindwa na Yeye mwenyewe.