Home
Categories
EXPLORE
True Crime
Comedy
Society & Culture
Business
Sports
TV & Film
Technology
About Us
Contact Us
Copyright
© 2024 PodJoint
00:00 / 00:00
Sign in

or

Don't have an account?
Sign up
Forgot password
https://is1-ssl.mzstatic.com/image/thumb/Podcasts114/v4/33/77/b3/3377b3b7-5a59-147a-a586-3abb04edd01b/mza_4028292745786506046.jpg/600x600bb.jpg
Msasa Media
Msasa Media
66 episodes
6 days ago
Msasaonline inaamini kila binadamu ana haki ya kuhabarika kuburudika, na kuelimika hivyo basi kazi yetu kuhakikisha tunakuletea habari sahihi, na kupunguza msongo wa mawazo kwa burudani nzuri na kubadirisha maisha yako kwa kuleta episode zenye mafunzo zaidi. Kwa undani zaidi tembelea web site yetu www.msasaonline.co karibu jisikie huru kuungana nasi.
Show more...
Daily News
News
RSS
All content for Msasa Media is the property of Msasa Media and is served directly from their servers with no modification, redirects, or rehosting. The podcast is not affiliated with or endorsed by Podjoint in any way.
Msasaonline inaamini kila binadamu ana haki ya kuhabarika kuburudika, na kuelimika hivyo basi kazi yetu kuhakikisha tunakuletea habari sahihi, na kupunguza msongo wa mawazo kwa burudani nzuri na kubadirisha maisha yako kwa kuleta episode zenye mafunzo zaidi. Kwa undani zaidi tembelea web site yetu www.msasaonline.co karibu jisikie huru kuungana nasi.
Show more...
Daily News
News
Episodes (20/66)
Msasa Media
"COUNTRY BOY" AZUNGUMZIA UMUHIMU WA MSANII KUWA TRENDING YOUTUBE NA VIEWS WENGI KWENYE MUZIKI WAKE.
"COUNTRY BOY" AZUNGUMZIA UMUHIMU WA MSANII KUWA TRENDING YOUTUBE NA VIEWS WENGI KWENYE MUZIKI WAKE.
Show more...
5 years ago
37 minutes 40 seconds

Msasa Media
Msani BELL 9 azungumzia wimbo aliowahi kuufanya wenye historia kubwa sana kwenye maisha yake.

Karibu sana endelea kupata burudani ya connection vibes ya Msasaonline. Ukibonyeza www.msasaonline.co utafurahia show

Show more...
5 years ago
31 minutes 49 seconds

Msasa Media
AY AFUNGUKA MAMBO MAKUBWA KUHUSU MZIKI WA BONGO FLAVOR
wwwmsasaonline.co
Show more...
5 years ago
31 minutes 44 seconds

Msasa Media
SABABU YA HUSSEIN MACHOZI KUJA TANZANIA

KARIBU KWA MARA NYINGINE TENA KWENYE MWENDELEZO WA EPISODE ZA CONNECTION VIBES

KIUNDANI ZAIDI BONYEZA www.msasaonline.co

ili uweze kuala unapatamwendelezo subscribe

Show more...
5 years ago
35 minutes 40 seconds

Msasa Media
MAONI YA ROSA REE KUHUSU MAPENZI

KARIBU SANA UBURUDIKE NA CONNECTION VIBES YA MSASAONLINE

KWA TAARIFA NA BURUDANI TEMBELEA  WWW.MSASAONLINE.CO

Show more...
5 years ago
1 hour 51 minutes 56 seconds

Msasa Media
CONNECTION VIBES

KARIBU UBURUDIKE NA CONNECTION VIBES

Show more...
5 years ago
37 minutes 50 seconds

Msasa Media
UHUSIANO ULIOPO KATI YA KAZI NA WITO.
Haijalishi uko wapi, unaishi wapi, wewe ni nani na unafanya nini. Ila ukweli ni kuwa kila mmoja wetu ana masaa 24 kwa siku. Na katika masaa hayo hayo tunatumia kwa kupumzika na kufanya mambo mbalimbali katika maisha. Moja kati ya maswali mwanadamu amekua akijiuliza mara kwa mara, ni kutaka kufahamu dhumuni la maisha yake hapa duniani. Tumekua tukijiuliza mimi ni nani? kwanini nipo hapa duniani?.Na katika kutafakari huko ndipo wengi wetu tunafikiria kuhusu kazi au wito wetu. Kwani kuna utofauti mkubwa uliopo kati ya KAZI na WITO. 1. KAZI. Neno "KAZI" linawakilisha aina ya huduma unayoitoa kwa mabadilishano. Kwa kufanya kazi unakua unatoa muda wako, juhudi, ujuzi, umakini, maarifa na ufahamu wako kwaajili ya kujipatia kipato. Na kitendo hiki ndo kinajulikana kama AJIRA, BIASHARA, POSHO. Unaweza kuwa na sababu nyingi za kwanini kila siku unaenda kufanya kazi. Lakini kama haupo huru kifedha , kujiingizia kipato ndio azimio kuu la kazi. 2. WITO. Neno "WITO" linawakilisha maslahi ya mtu binafsi, kile anachopenda, kinachomvutia na kumsukuma mtu. Wito sio kitu unachohitaji kukifanya, hiki ni kitu chenye msukumo mkubwa ndani yako. Lakini licha ya hivyo wito unaweza kukuingizia kipato au ikawa kazi pia wakati huohuo. Wito unaweza kuja Kupitia njia mbalimbali mfano Sanaa, Usafi, au shughuli zozote za kibunifu (mfano Uandishi au uchoraji). Lakini licha ya hivyo WITO wa kweli na wenye nguvu ni ule wa kiutumishi. Na kupitia wito huu ndipo utakutana na huduma kadhaa za kujitolea mfano kufundisha, kufanya kazi kwa pamoja, kutoa misaada mbalimbali. Hapo ndio utajua utofauti wa KAZI na WITO. KAZI : ni kwaajili ya kipato. WITO : ni kwaajili ya utoshelezi. Lakini inaweza kutokea unaipenda sana kazi yako mpaka upo tayari kufanya hata bure, basi hapo hubalika na kuwa WITO na sio KAZI. na ikiwa wito itaanza kuzalisha faida.
Show more...
5 years ago
2 minutes 31 seconds

Msasa Media
SIRI ZA MAFANIKIO YA MTU BINAFSI.
Neno mafanikio kila mtu huwa ana maana yake kwa wakati wake na kwa eneo lake katika maisha. Nikiwa na maana kuwa kila mtu ana tafsiri yake kuhusu mafanikio kutokana na muda na wakati alionao na anaoendelea kuishi hapa duniani. Mfano : kuna mafanikio ya kiafya, kiuchumi, kiuchumi, kimahusiano. Sasa katika makala yetu leo hii tutazungumzia zaidi juu ya Mafanikio ya kiuchumi na kifedha. Hizi ni Siri muhimu ambazo ni nguzo kuu za kukusaidia kufikia Mada makubwa kiuchumi na kifedha. 1. IMANI NA IBADA. Siku zote hakuna njia ya kufanikiwa kirahisi bila ya kuwa na imani na kufanya ibada, na ndio maana kuna watu wanashinda kwenye nyumba za ibada wakimuomba Mungu huku wengine wakikesha kwa waganga kutokana na imani yao ili kupata utajiri na mali. Lakini nikwambie tu MFANIKIO ya kweli na yenye furaha ni yale utakayoyapata kutokana na kumuamini mwenyezi Mungu pekee. Jifunze kufanya ibada kila mara na utambue kuwa binadamu sio kazi ya mikono yake pekee bali ni kazi inayotokana na Mungu pekee na kila binadamu ana fungu lake jema mbele ya mwenyezi Mungu aliye muumba. 2. KUFANYA KAZI KWA BIDII. Suala zima la kufanikiwa katika maisha linahitaji kujitoa kila mara na kufanya kazi kwa bidii hasa. Kwani kufanya kazi kwa bidii huendana na ufanisi na ujuzi wako ulionao. Acha kuwa mtu wa kulalamika sana na kukata tamaa mapema, bali anza sasa kujituma utaona mafanikio mapema sana. 3. KUWA MSOMAJI ZAIDI. Kusoma mambo mbalimbali yanayohusu maisha au kile kitu ulichowekeza katika maisha yako kukifanya, hiyo ni sehemu tosha inayoweza kukubadilisha fikra zako na kukufanya kuwa bora na kuwa mtaalamu au mfanisi mkubwa katika utafutaji wa mafanikio yako. Kusoma sio mpaka urudi darasani, ila nina maana kuwa UJIFUNZE kusoma hata mambo hata yale ya kawaida yanayohusu maisha na mafanikio binafsi. Anza kusoma vitabu mbalimbali vinavyohusu maendeleo ya mtu binafsi, utajiri, kuwekeza, afya, usafi, ufanisi wa kazi au masoko. Mfano vitabu kama Rich Dad poor Dad, Maximum Achievement, The power of positive thinking au Self Billionaire. 4. MAHUSIANO MZURI NA WATU. Kuwa na mahusiano na watu wako wa karibu ni jambo jema linaloweza kukuweka katika mazingira mazuri zaidi ya mafanikio makubwa na ukawa mtu wa tofauti na wengine katika nyanja za maisha. Kama usipokua na mahusiano mazuri na watu basi swala la kukosa furaha na amani kwako itakua ni la kawaida sana. 5. KUWA NA NIDHAMU YA MUDA. Muda ndio msingi mzuri na wa kipekee wa kukusaidia kufikia malengo yako uliyojiwekea. Huwezi kufikia mafanikio makubwa kama bado hauna nidhamu kwenye swala la muda. Jifunze kwenda na muda ili uongeze ubora katika kazi yako, heshima yako na nidhamu yako binafsi. 6. NIDHAMU YA MATUMIZI YA FEDHA. Ukishindwa kutumia fedha zako vizuri na kujiwekea akiba basi hesabu kuwa wewe utakuwa unafanya jambo ambalo halina mwisho wake. Kutokua na nidhamu ya fedha ni kama vile unataka kuanzisha safari bila kujua mwisho wake ni nini. 7. KUJIAMINI NA KUJIKUBALI BINAFSI. Kujiamini ni hali pekee ndani ya mtu ya kuwa jasiri bila uongo katika jambo lolote lile analolikabili mbele yake. Ukijiamini na kujikubali wewe mwenyewe itakua ni rahisi na wengine kukuamini.
Show more...
5 years ago
3 minutes 57 seconds

Msasa Media
NAFASI YA TAALUMA NA NIDHAMU KWENYE JAMII.
Nidhamu ni utii, kusikia, na kusikiliza. Nidhamu ni kufuata sheria, kanuni na taratibu kutoka kwa wanaokuongoza. Nidhamu ni kuwa mahala sahihi, wakati sahihi na kufanya jambo lililokuhitaji kuwa mahala pale kwa wakati ule. Nidhamu sio shikamoo, nidhamu sio upole na nidhamu sio Mavazi yenye staha pekee. Nidhamu ni zaidi ya mwonekano nadhifu na mavazi adili. Nidhamu ni mwenendo chanya, tabia nzuri, fikra chanya na kauli jengefu. Taaluma ni maarifa, ujuzi na mjongeo fulani wa fikra unaokuwa umepangiliwa utolewe kwa wanaojifunza ili wawe wataalamu ktk ugha fulani. Taaluma ni mafunzo yatolewayo kwa kufundisha wanafunzi ili wawe wataalamu wa kada fulani ktk jamii au Taifa. Mfano, Taaluma ya Umeme ni matokeo ya kufundishwa na kujisomea ktk mazingira rasmi na kufuata taratibu rasmi ili kuweza kuhitimu masomo ya UHANDISI wa UMEME na kujiajiri au kuajiriwa kama mtaalamu wa UMEME. NIDHAMU NI TAALUMA. Hakika, awae mwanajeshi huwa na nidhamu.Awae nurse au Daktari huwa na nidhamu na Awae padre huwa na nidhamu. Nidhamu hupaswa kuwa nayo kabla, wakati na baada ya kuhitimu elimu ya Taaluma fulani. Nidhamu sio jambo la Mda ingawaje Wanadamu tumeumbiwa kujisahau au hisia(mood). Hii huleteleza hasira, chuki na wakati mwingine kukengeuka na kujikuta Daima tunafanya au Tunasaka taaluma tukiwa watovu wa nidhamu mbele ya watoaji wataaluma tuliopaswa kuwaheshimu na kuwaonesha nidhamu kila mawio na machweo ya elimu tuitafutayo. Taaluma ni nidhamu. Ili mtoto afanye vyema ktk Taaluma yake, yaani ufaulu maridhawa Itampasa kuwa msikivu(nidhamu), mtulivu(nidhamu), mfuata maelekezo(nidhamu), mhudhuriaji shuleni(nidhamu), msomaji na mfanyaji wa mitihani(nidhamu) huku akiambatanisha na tabia, mienendo na maadili mema(nidhamu).
Show more...
5 years ago
1 minute 48 seconds

Msasa Media
PAUL POGBA AKUTWA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA CORONA.
Kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps amesema kiungo wa kati wa klabu ya Manchester United, Paul Pogba amepatikana na maambukizi ya Virusi vya Corona. Kutokana na taarifa hiyo Pogba mwenye umri wa miaka 27 atalazimika kujitenga na wachezaji wenzake ambao wapo kwenye maandalizi ya michuano ya ligi ya Taifa la Ufaransa. Kwahiyo mfaransa huyo atakosa mechi ya kitaifa ya Ufaransa itakayochezwa siku ya Jumamosi tarehe 5 Septemba, 2020 na siku 3 baadae atakosa kwenye mechi dhidi ya Crotia. Hata hivyo Pogba huenda akachaguliwa katika uteuzi wa timu ya ufunguzi Manchester United dhidi ya Crystal Palace kwenye ligi kuu ya Uingereza ndani ya uwanja wao wa Old Trafford. Vile vile baada ya kuenea kwa taarifa ya kuambukizwa Corona, klabu ya ya Manchester United na Wachezaji wenzake wamemtakia heri ya kupona haraka kabla ya kuanza kwa msimu. Ila nafasi ya Paul Pogba katika kikosi cha Ufaransa itachukuliwa na kiungo wa kati wa Rennes Eduardo Camavinga mwenye asili ya Angola, anaecheza Klabu ya Stade Rennais FC.
Show more...
5 years ago
1 minute 28 seconds

Msasa Media
CLOUDS TV NA REDIO ZAFUNGIWA KWA SIKU 7.
MAMLAKA ya Mwasiliano Tanzania (TCRA) imeagiza Clouds TV na Redio kusitisha matangazo yao kwa muda wa siku saba kuanzia kesho Ijumaa 28 Agosti hadi 3 Septemba 2020 kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji na kanuni ndogo za utangazaji za uchaguzi. Pia, mamlaka hiyo imevitaka Clouds TV na Redio kuomba radhi siku nzima ya leo Alhamisi tarehe 27 Agosti 2020 kwa kosa hilo. Akizungumza na waandishi wa habari makamo makuu ya mamlaka hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba amesema, adhabu hiyo inatokana na kukiuka kanuni mbalimbali za utangazaji na kanuni ndogo za wakati wa uchahuzi za mwaka 2015. Kilaba amesema, Clouds TV na Redio walikiuka kanuni za utangazaji kwa kutangaza wagombea kupita bila kupingwa wakati wenye uwezo wa kutangaza ni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). "Mnamo tarehe 26 Agosti 2020 kati ya saa 1 hadi 4 asubuhi kupitia vipindi Clouds 360 na Powerbreakfast Clouds Redio. Walirusha takwimu za wagombea ubunge waliopita bila kupingwa lakini wakijua taarifa hiyo haijathibitishwa na NEC na kukosa pia midhania," amesema Kilaba. Kutokana na ukiukwaji huo, Kilaba amesema, “kuanzia muda wa agizo hili saa 8 mchana leo mpaka mwisho wa siku hii ya leo, Clouds TV wanatakiwa kuahirisha matangazo yote na kutumia muda wote uliobaki kuomba radhi kwa Watanzania wote kwa kukiuka kanuni ya utangazaji kupitia kipindi chao cha Clouds 360." “TCRA imesitisha utoaji wa huduma za utangazaji kwa Clouds TV kuanzia kesho 28 Agosti 2020 hadi 3 Septemba 2020. Yaani hakuna kwenda hewani. Iwapo Clouds TV itashindwa au itakaa au itakaidi uamuzi huu, hatutakuwa na jinsi nyingine, tutachukua hatua zingine za kisheria na kithidhibiti,” amesema Kilaba amesema, maagizo hayo kwa Clouds Tv yanafanyika pia kwa Clouds Redio kwa muda huo huo. “Iwapo Clouds Redio itashindwa, itakaa au kukaidi, basi TCRA itachukua hatua za kisheria kati yao,” amesema Kilaba Mkurugenzi huyo amesema, “kwa kipindi chote cha uchaguzi, tuzingatie sheria na hii ni kwa vyombo vyote vya habari na pia zile za online.” Pia, Kilaba ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii hususan makundi, “wananchama wa vyama vyote vya siasa kuzingatia matakwa ya kisheria kuhusu masuala ya uchaguzi tunapohusisha mitandao ya mawasiliano."
Show more...
5 years ago
2 minutes 51 seconds

Msasa Media
KENYA: MUDA WA WANANCHI KUTOTOKA NDANI WAONGEZWA KWA SIKU 30.
Katika jitihada za kudhibiti maambukizi ya Covid-19, Rais Uhuru Kenyatta ameongeza muda wa wananchi kutotoka ndani kuanzia saa 3 usiku hadi saa 10 alfajiri kwa siku 30. Akihutubia Taifa kutoka Ikulu, amesema baa zitaendelea kufungwa kwa siku 30 huku akiagiza Wizara ya Afya kukutana na wamiliki ili kupata muongozo sahihi wa kuzifungua. Aidha, Rais Kenyatta ameongeza idadi ya watu wanaoweza kuhudhuria misiba na harusi kutoka 15 iliyokuwepo awali hadi 100.Migahawa itafungwa saa 2 usiku baada ya saa 1 usiku kuanzia kesho. Pia, Rais amezitaka Wizara za michezo na Afya kuandaa miongozo ya pamoja ili kurejesha shughuli za michezo nchini humo. Kama utakumbuka siku mbili zilizopita ndani ya Taifa hilo kulikuwa na taarifa za madarasa ya shule binafsi kwasasa yanatumiwa kufugia kuku kutokana na shule kufungwa mpaka mwezi Januari, 2021. Kenya imerekodi visa 33,016 na vifo 564 huku idadi ya wagonjwa waliopona ikiwa 19,296.
Show more...
5 years ago
1 minute 37 seconds

Msasa Media
NEW ZEALAND : ALIYEUA WAUMINI 51 MSIKITINI AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA.
Mahakama imemhukumu kifungo cha maisha jela bila uwezekano wa msamaha Brenton Tarrant(29) aliyeua watu 51 kwenye misikiti miwili nchini humo.mtoto mwenye umri wa miaka 3 alikuwa miongoni mwa waliouawa. Machi mwaka jana, waumini waliokuwa wanasali katika msikiti wa Al Noor na Linwood walishambuliwa na Tarrant ambae alirusha tukio hilo mubashara Kupitia mtandao wa facebook. New Zealand haina adhabu ya kifo na Jaji Cameron Mander amesema hukumu hiyo hutolewa kwa wauaji wabaya zaidi,akiongezea kuwa kitendo kilichofanywa na mtuhumiwa hakikuwa na ubinadamu. Hii ni kwa mara ya kwanza kwa hukumu ya aina hiyo kutokewa katika historia ya New Zealand.Mtuhumiwa ambae ni raia wa Australia alikiri kufanya mauaji hayo na kujaribu kuuwa wengine 40.
Show more...
5 years ago
1 minute 17 seconds

Msasa Media
MCHEZAJI WA VALENCIA "DANI PAJERO" AMWAGA MACHOZI BAADA YA KUTEMWA NA TIMU YAKE.
Mchezaji wa muda mrefu ndani ya klabu ya Valencia, Dani Pajero amejikuta akitokwa na machozi baada ya kupigwa chini na klabu yake ya Valencia, na sasa ataichezea klabu ya Villarreal ambao ni wapinzani wa Valencia. Kiungo huyo wa kati wa Uhispania amecheza Valencia mechi 383 tangu mwaka 2008 alipojiunga na klabu hiyo akitokea Getafe, na mwaka 2011 alikaririwa akisema kuwa ndoto yake ni kuja kustaafu klabuni Hapo, lakini kwa bahati mbaya ameshawekwa pembeni. Itakumbukwa Pajero alifanikiwa kuiongoza Valencia Kwenye ubingwa wao wa kwanza tangu 2008, wakati aliposhinda kikombe cha Copa Del Ray msimu wa 2018 / 2019. Vilevile nchini Hispania klabu ya Atletico Madrid imeondolewa kwenye mashindano ya klabu bingwa Ulaya baada ya kufungwa magoli 2 - 1 dhidi ya RB Leipzig kwenye hatua ya robo fainali na kuifanya klabu hiyo ya Ujerumani kuandika historia ya kuingia nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu ilipoanzishwa mwaka 2009. Kocha wa RB Leipzig, Julian Nagelsman nae ameingia kwenye historia ya kuwa kocha wa kwanza mdogo (miaka 33) aliewahi kufika kwenye nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Show more...
5 years ago
1 minute 34 seconds

Msasa Media
CHINA : NYAMA YA KUKU YAKUTWA NA VIRUSI VYA CORONA.
Sampuli ya vipapatio / mabawa ya kuku yaliyogandishwa, zimegundulika kuwa na virusi vya Corona mjini Shenzhen. Nyama hizo ziliagizwa kutoka nchini Brazil. Baada ya ugunduzi huo, mamlaka za afya ziliwatafuta na kuwapima watu waliokuwa karibu na bidhaa hiyo ambapo majibu yamesema kuwa hawana maambukizi. Aidha eneo ambalo vipande vyenye virusi viliwekwa limepuliziwa dawa na mamlaka inatafuta bidhaa zingine za kampuni hiyo ambayo bado haijawekwa wazi. Hata hivyo shirika la Afya Duniani (WHO) na kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Marekani (CDC) zimewahi kusema uwezekano wa kupata Corona ni mdogo kupitia chakula. Taarifa hiyo ya kupatikana kwa Covid-19 kwenye mabawa ya kuku, imekuja huku siku moja tu nyuma yake nchini Ecuador kulipatiana virusi vya Corona kwenye samaki wadogo wa baharini aina ya uduvi wakiwa kwenye moja kati ya migahawa nchini humo kwaajili ya kuuzwa kwa wateja. Mpaka sasa taifa la China limeripoti kuwa na visa 84,786, huku Brazil ikiwa na nchi ya pili kuwa na maambukizi makubwa ya Covid-19, kwa kuwa na visa Milioni 3.1 na taifa la Marekani likiwa linaongoza kwa kuwa na visa Milioni 5.26
Show more...
5 years ago
1 minute 31 seconds

Msasa Media
LINAH : "MIMI NA MORRISON SIO WAPENZI, NI MARAFIKI TU".
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Linah Sanga (Linah) ameamua kuuvunja ukimya baada ya kusambaa taarifa za kuwepo na mahusiano ya kimapenzi kati yake na mchezaji wa Simba, Benard Morrison. Ule msemo wa "uongo ukiachwa ukasambaa kwa ukubwa zaidi, huwa unageuka ukweli" umejaribu kupingwa vikali na mrembo huyo na kusema kuwa, Yeye na Benard Morrison Ni washkaj tu na wala hakuna mapenzi yoyote yanayoendelea kati yao kama watu wanavyodhani. Linah akaongezea kwa kusema, "yeye ni shabiki yake na mimi ni shabiki yake, tulikutana kwenye mazingira fulani ambayo hata mimi sikutegemea kama ningekuwa hapo, kwani alivyoniona alisema ni mwanamuziki anaefatilia kazi zangu tangu muda mrefu sana, na hata alivyoniita nikaingia hiyo sehemu aliyekuwepo alikua anacheza game na washkaj zake,basi tukapiga picha. Mpenzi wa msasa online kama utakua unakumbuka Msanii Linah mara kadhaa ameshaingia kwenye taarifa za ku'date na watu maarufu, kwa mfano alishawahi kupiga picha za ukaribu na mchekeshaji Idriss Sultan ambapo baadae ikajulikana ilikua ni kutengeneza kiki ya ujio wa wimbo wake wa raha jipe mwenyewe. Benard Morrison hivi karibuni aliingia vichwa vya habari vya nchini Tanzania, baada ya kushinda shauri lake dhidi ya klabu ya Yanga aliyokua anaichezea hapo awali.
Show more...
5 years ago
1 minute 39 seconds

Msasa Media
IRAN : YATISHIA KUCHUKUA HATUA KAMA MARUFUKU YA SILAHA ITAREFUSHWA.
Rais wa Iran Hassan Rouhani ametishia kuwepo na madhara iwapo baraza la usalama la umoja wa Mataifa litarefusha marufuku ya silaha dhidi ya Iran kwa shinikizo la Marekani. Rouhani amesema kupitia televisheni ya taifa, kwamba azimio nambari 2231 la umoja wa Mataifa, ambalo ni sehemu ya makubaliano ya nyuklia yaliyofikiwa mjini Vienna mwaka 2015 linahitaji marufuku hiyo iondolewe ifikapo mwezi Oktoba. "Hivi sasa wamarekani wamependekeza azimio dhidi ya sehemu ya azimio nambari 2231 ili kulikiuka. Tuna matumaini makubwa kwamba Marekani itashindwa. Tuna matumaini makubwa tena, kwamba Marekani itagundua kushindwa kwake na kushuhudia kutengwa kwake, amesema Rouhani. Marekani ilijitoa kwenye makubaliano hayo mei 2018,na baadae utawala wa Trump ukaiwekea Iran vikwazo zaidi. Makubaliano hayo yamekabiliwa na kitisho cha kuvunjika, kwa sababu Mataifa yaliyosalia China, Ufaransa, Uingereza, Urusi na Ujerumani, hayawezi kutekeleza sehemu ya kiuchumi ya makubaliano kukiwa na vikwazo vya Marekani,hali iliyoisukuma Terhan pia kuanza kuyakiuka.
Show more...
5 years ago
1 minute 26 seconds

Msasa Media
TABIA ZA WATU WENYE USALITI KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI.
Usaliti ni jambo baya sana katika mahusiano, usaliti si ujanja japo wengi wanaowaza kusaliti huwa wanajiona wajanja.wanajiona wamefanikiwa pale ambapo wanasaliti wenza wao kutogundua kama wanasalitiwa. Siku zote anaekusaliti huwa anajiona mjanja sana, kwamba yeye anasaliti mwenza wake hasaliti. Kwa asilimia kubwa wanaume hujiona kama usaliti ni halali yao, wanataka wao wasaliti lakini wapenzi nb wao wasithubutu kuwasaliti. Kwanini hawataki wenza wao wasaliti? eti wanaumia, hakuna kitu kinacho mchukiza mwanaume kama kusalitiwa. kusaliti asaliti yeye akisaliti mwenzake ni kosa la jinai anaona amedhalilishwa Anajisikia fedheha kwamba Mpenzi wake amemuonaje? amemchukuliaje?hajakamilika idara gani? Anawaza sana na kujiuliza jamii nzima inayojua kitendo hicho inamtazamaje?. Hapo ndio unakuta mwanaume anaamua kuchukua uamuzi mgumu ikiwemo hata kuhatarisha maisha ya mwenza wake. Zifuatazo ni dalili za usaliti. 1. KUTOPENDA KUFATILIWA KIUNDANI. Mara nyingi anaekusaliti hapendi kuchimbwa mambo kwa undani, anahofu anaweza kuchanganya madawa, hapendi mazungumzo mafupi ya moja kwa moja. Hapendi kuulizwa maswali mengi, ukimuuliza anayakwepa na kutaka kukupeleka kwenye mazungumzo anayoyataka yeye. Ukimuuliza Kuhusu mipango yenu, ukimuuliza Kuhusu mustakabali wa mahusiano yenu hawezi kukujibu moja kwa moja baada huku ondoa kwenye mstari na kukufanya usiwe na hamu ya kumuuliza. 2. HAPENDI UJUE RATIBA ZAKE. Mara nyingi mtu ambaye ana mambo yake hapendi ujue ratiba zake, anataka usimzoee ,iwe anafanya maamuzi yake kulingana na yeye mwenyewe anavyotaka, ikitokea unaijua ratiba yake atakuwa ni mtu wa kutoa udhuru kila wakati. Leo atakwambia kuna mgonjwa anakwenda kumuona, kesho atakwambia kuna kikao cha wafanyakazi wenzake, siku nyingine atakwambia gari imepata pancha analazimika kusubiri mafundi hadi wafike ndio aweze kuanza safari. 3. SIMU YAKE NI KITUO CHA POLISI. Anayesaliti mara nyingi hapendi kuacha simu yake kiholela, simu inakaa mfuko kwake hata kama hakuna ulazima wa kufanya hivyo mpo nyumbani kwenye kikao cha mazungumzo ya kifamilia yeye simu yake ipo mfukoni. Imetolewa mlio hataki usikie ikiita, au ujumbe ukiingia ,au picha na mambo mengine ya kimapenzi. Anayejiamini na yupo kwenye uhusiano imara hana sababu ya kuficha ficha simu yake au kuweka paswedi kila mahali simu yake anaiweka hadharani. Mwingine anakusetia simu yake ukimpigia kila wakati inaonekana inatumika wakati huo anakusaliti. 4. ANACHATI SANA. Wanaosaliti wengi wao hupenda kutumia meseji katika mawasiliano yao, yaani anawazoesha michepuko yake wote kusaliti hapendi kupokea simu zaidi anapenda kuchati hivyo ni rahisi kuchati na wapenzi wengine bila wewe kujua na kufuta meseji zote ili hata ukishika simu kwa bahati mbaya usizione na usigundue kitu. Mwisho hakutambulishi kwa watu wake wa karibu, ukiona mpenzi wako hajawahi kukutambulisha kwa rafiki zake, ndugu zake na watu wengine wa karibu ujue hapo hamna muelekeo wa mapenzi yenu tafuta njia mapema ya kujiundoa kabla ya kupotezewa muda wako. Kwa haya machache natumaini utakuwa umeshafahamu Mpenzi wako uliyenae kwa sasa ana malengo gani? na je anakusaliti ama ni mwaminifu ili uweze kuchukua hatua mapema kabla mambo hayajaharibika.
Show more...
5 years ago
3 minutes 40 seconds

Msasa Media
FAIDA 8 ZA KUWEKA AKIBA UNAZOPASWA KUZIFAHAMU.
1. Uhuru wa kifedha. Uhuru wa kifedha ni zaidi ya kuwa na fedha, uhuru wa kifedha ni kuwa mtu ambaye unatakiwa kuwa maishani na kuweza kufanya au kupata kile unachokihitaji maishani. Hata hivyo pesa ni muhimu sana kwenye suala la uhuru wa kifedha,ingawa pesa hizi zinatakiwa ziambatane na fikra sahihi. Kwa njia ya kujiwekea akiba utaweza kujijengea msingi mzuri wa kifedha ambao ukiambatanishwa na fikra sahihi utakuletea uhuru wa kifedha. 2. Matumizi mazuri ya pesa. Kama nilivyoeleza hapo mwanzo kuwa kuweka akiba sio kuwa na pesa nyingi bali ni maamuzi na mipango stahiki pekee. Hivyo kuweka akiba kutakufaidisha kwa kukuwezesha kutumia pesa vyema.ikiwa unapata elfu 10 kwa siku,itakubidi uitumie vizuri ili uweze kutenga pesa ya akiba. Kama huweki akiba huna haja ya kutumia pesa vyema kwani hakuna sehemu ya akiba inayotakiwa kutengwa. 3. Kujiandaa kwa dharura Watu wengi huingia kwenye madeni au kupata uhitaji mkubwa wa pesa mara wapatwapo na dharura. Hivyo kwa kuweka akiba utapata faida ya kukuepushia mahangaiko wakati wa dharura kama vile magonjwa, misiba majanga n.k 4. Kuweza kufanya manunuzi au miradi ya gharama kubwa Kuna manunuzi au miradi inahitaji pesa nyingi ili kuitekeleza. Maswala kama vile ujenzi wa nyumba, ununuzi wa viwanja kununua gari n.k, ni baadhi ya mambo yanayohitaji fedha nyingi. Hivyo,kwa kuwa na akiba utaweza kutekeleza mambo haya kwa urahisi kuliko ungeyafanya bila akiba. 5. Kuweza kumudu wanaokutegemea Ikiwa kuna watu wanaokutegemea kama vile wazazi, ndugu au watoto ni vyema kuweka akiba ili uwe na fedha ya kukidhi mahitaji yao mara wapatwapo na uhitaji. Kutokuweka akiba kutakufanya uhangaike huku na huko ili kutafuta pesa ya kukidhi mahitaji ya wategemezi wako kama vile chakula, matibabu au hata ada za shule. 6. Utulivu wa akili Unapokuwa huna akiba yoyote huwezi kuwa na utulivu wa akili, Kila wakati unahofu na wasiwasi juu ya maisha yako, unajiuliza likitokea tatizo itakuwaje? au hitaji fulani linalokuja hivi karibuni itakuwaje?n.k Unapokuwa na fungu fulani la akiba huna haja ya kuwa na wasiwasi kwa unajua hata ukikosa pesa akiba yako itakusaidia. 7. Hukuwezesha kuandaa kesho vyema Maandalizi ya kesho yanafanywa leo.kuweka akiba maana yake unajiandaa na mahitaji ya kifedha ya baadaye yaani kesho.mtu asiye kuwa na akiba mara nyingi hafikirii Kuhusu kesho wala hamna malengo kwa ajili ya baadaye yake. Ili kujenga baadae au kesho njema,ni muhimu pia kuimarisha msingi wako wa kiuchumi kwa njia ya kuweka akiba. 8. Hukuwezesha kuwahi fursa Ni mara ngapi umekuwa ukisema au ukisikia kauli kama vile" ningekuwa na pesa ningenunua hiki kitu",au "ningekuwa na pesa ningejiunga kwenye hii huduma" au "ningekuwa na pesa ningejiunga kwenye huu mradi".n.k Hili kinadhihirisha watu hukosa fursa mbalimbali kutokana na kukosa akiba ya pesa,unapokuwa na akiba ya pesa ni rahisi kuwahi fursa mpya au bidhaa zenye manufaa mara zinapopatikana. Hitimisho Fedha ni jambo linalohitaji nidhamu na busara ya hali ya juu, vivyo hivyo kuweka akiba ni swala linalohitaji kufanya maamuzi sahihi ili uweze kulitekeleza.
Show more...
5 years ago
3 minutes 34 seconds

Msasa Media
MWINYI ZAHERA ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI GWAMBINA FC.
Mwinyi zahera ametambulishwa rasmi kuwa kocha Mkuu wa klabu ya Gwambina FC ambayo imepanda daraja msimu wa 2019/20 na itashiriki ligi kuu Bara msimu wa 2020/21. Zahera aliwahi kuifundisha yanga ndani ya ligi msimu wa 2018/19 na alianza nayo msimu wa 2019/20 kabla ya kufungashiwa virago kwa kile kilichoelezwa kuwa aliboronga kwenye michuano ya kimataifa. Kocha huyo amesaini dili la miaka 5 na inaelezwa kuwa ataanza kusajili nyota wake ambao alifanya nao kazi ndani ya Yanga. Wanaotajwa kuibukia Gwambina ni pamoja na Mrisho Ngassa na Kelvin Yondani ambao kwa sasa ni wachezaji huru. Vilevile Waziri wa michezo Tanzania, Dkt Harison Mwakyembe ametangaza uamuzi wa serikali kuendelea kuruhusu idadi ya wachezaji 10 wa kigeni huku idadi ya wachezaji wanaotakiwa kucheza itaratibiwa chini ya baraza la Michezo la Taifa BMT. Amesema bado wizara kwa kushirikiana na BMT na wadau wa soka watakaa kikao kujadili aina ama viwango vya wachezaji wanaopaswa kusajiliwa na kuingia nchini. Amefafanua, "Angalau nchi zilizopo katika nafasi 50 kwa FIFA ndiyo tusajili huko hata kwa daraja la kwanza, ingawa bado hii si sheria ni maoni tuu,ni vyema pia aina ya wachezaji watakaosajiliwa kutoka nje wawe na weledi na uwezo mkubwa.
Show more...
5 years ago
1 minute 36 seconds

Msasa Media
Msasaonline inaamini kila binadamu ana haki ya kuhabarika kuburudika, na kuelimika hivyo basi kazi yetu kuhakikisha tunakuletea habari sahihi, na kupunguza msongo wa mawazo kwa burudani nzuri na kubadirisha maisha yako kwa kuleta episode zenye mafunzo zaidi. Kwa undani zaidi tembelea web site yetu www.msasaonline.co karibu jisikie huru kuungana nasi.